Machapisho

Inaonyesha machapisho kuanzia Septemba, 2017

VISHETI

Picha
Mahitaji:- Unga wa ngano kg 1 Mafuta ya kupikia lita 1 Siagi robo kg Nazi iliyo kunwa (machicha) susu kikombe Sukari nusu kg Iliki kijiko cha chai Backing powder vijiko viwili vya chai Maji kiasi Matayarisho:- Weka unga wako kwenye bakuli  Weka nazi yako iliyokunwa (machicha) Weka iliki Weka siagi Weka backing powder Changanya mchanganyiko vyote vichanganyikie kwenye unga Weka maji kiasi kuchanganya upate donge la unga Maji yasiwe mengi unga ukatota Kanda unga kidogo tuu ili maji yachanganyike vizuri Unga ukisha kua mlaini kata kata madonge  Sukuma madonge kwenye kibao cha chapati iwe kama chapati Sukuma na unga mkavu kidodo ili madonge yasishike kwenye kibao Chukua kisu ukate dizain ya visheti  Bandika mafuta ya kula jikoni Yakipata moto kaanga visheti ulivyo katakata  vivve na kupata rangi ya broun  Jinsi ya kuandaa sukari Weka sukari kwenye sufuria Iroweshe na maji kidogo sana  Bandika jikoni na moto mdogo sukari iyayuke na yale maji yakauke K

TAMBI ZA SUKARI

Picha
Mahitaji : - Tambi Sukari Mafuta ya kula Hiliki Maji Jinsi ya kupika:- Bandika mafuta yapate moto Kaanga tambi ziwe rangi ya udongo (broun) Chuja mafuta pembeni tambi zikishakua za rangi ya udongo (broun) Ukisha chuja mafuta  weka maji kiasi yasiwe mengi  Weka hiliki na sukari  Punguza moto kisha funikia maji yakauke na tambi zikauke kuiva   Kama maji yakikauka hazija iva ongeza maji kidogo kidogo mpaka ziive.  Chunga usiweke maji mengi zikatota Maji yakisha kaukia, tambi zikiiva zitakua tayari kuandaa kwa kula