VISHETI

Mahitaji:-

  • Unga wa ngano kg 1
  • Mafuta ya kupikia lita 1
  • Siagi robo kg
  • Nazi iliyo kunwa (machicha) susu kikombe
  • Sukari nusu kg
  • Iliki kijiko cha chai
  • Backing powder vijiko viwili vya chai
  • Maji kiasi
Matayarisho:-
  • Weka unga wako kwenye bakuli 
  • Weka nazi yako iliyokunwa (machicha)
  • Weka iliki
  • Weka siagi
  • Weka backing powder
  • Changanya mchanganyiko vyote vichanganyikie kwenye unga
  • Weka maji kiasi kuchanganya upate donge la unga
  • Maji yasiwe mengi unga ukatota
  • Kanda unga kidogo tuu ili maji yachanganyike vizuri
  • Unga ukisha kua mlaini kata kata madonge 
  • Sukuma madonge kwenye kibao cha chapati iwe kama chapati
  • Sukuma na unga mkavu kidodo ili madonge yasishike kwenye kibao
  • Chukua kisu ukate dizain ya visheti 
  • Bandika mafuta ya kula jikoni
  • Yakipata moto kaanga visheti ulivyo katakata vivve na kupata rangi ya broun 

  • Jinsi ya kuandaa sukari
    • Weka sukari kwenye sufuria
    • Iroweshe na maji kidogo sana 
    • Bandika jikoni na moto mdogo sukari iyayuke na yale maji yakauke
    • Kisha tia visheti vilivyokaangwa na kuvirusha rusha ili kuvigeuza vya juu vije chini na vya chini vije juu sukari ienee kwenye visheti
    • Sukari ikisha ingia vizuri katika visheti na kukauka, viweke kwenye sinia au tray vipowe tayari kwa kula

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

TAMBI ZA SUKARI

Biriani (Biryani)